Quantcast
Channel: HANDENI KWETU
Viewing all 1305 articles
Browse latest View live

Karibu uangalie tamasha la Handeni Kwetu kwenye mtandao wa youtube na ufaidi kilichojiri

$
0
0
NDUGU mdau wa Blog hii, tunakuomba usikose kuangalia video ya Tamasha la Handeni Kwetu lililofanyika mwaka jana, Desemba 14 wilayani Handeni, mkoani Tanga.

Ingia kwenye Google, andika Youtube, kisha andika Tamasha la Handeni Kwetu 2013. Utaona uhondo huu ambao si wa kukosa kuutazama. Hii ni kazi mahususi iliyowekwa kwenye mitandao kwa ajili ya kukupatia wewe kuangalia kilichojiri katika tamasha hilo, ambalo litafanyika kila mwaka baada ya kuzinduliwa rasmi mwaka jana.

Usisite kutoa maoni yako popote ulipokuwapo juu ya video hiyo, tamasha hilo na mambo yote unayohisi unahitaji kuyajua. Karibu sana. email yetu ni kambimbwana@yahoo.com au +255712053949.

ASANTENI.

Yuko wapi mwimbaji wa 'Niite Basi', Joslin? Unakumbukwa na mashabiki wako popote ulipojificha

$
0
0
Joslin pichani.
WAPENZI wa muziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo Fleva, hawatashindwa kuufahamu wimbo wa 'Niite Basi'. Wimbo huu uliimbwa kwa ustadi mkubwa na msanii Joslin aliyekuwa ndani ya kundi la Wakali Kwanza.
Mr Blue pichani.
Kwa wadau haswa, jina hili ni tishio kwao maana linawagusa moja kwa moja juu ya kibao hiki. Ilikuwa balaa. Baada ya kutoka na wimbo huo, msanii huyu alitingisha katika vituo vya redio na televisheni.

Kila shoo alikuwa hakosi. Wengi wanapenda jinsi alivyoimba kwa hisia na mipangilio ya aina yake. Kwa mfano, katika mashairi yake kuna mahali anagusa zaidi anaposema; Unaponiita mpenzi Joslin napata wazimu, isitoshe baby pale unaponichumu, mwili unasisimka then napoteza fahamu babyyyyy, nitafanya nini? Haya ni baadhi ya mashairi makali sana.

Katika historia ya mapenzi kila mtu anajua namna gani anajisikia faraja kuwa na anayempenda kwa dhati. Fikiria mtu anakuita mpenzi au anakuchumu kabisa. Duhhh ni shidaaa.

Pamoja na mazuri haya, lakini msanii huyu alianguka kabisa. Hata pale alipotoa wimbo wake uliokwenda kwa jina la Itika haujaweza kumrudisha kileleni tena. Ule msuguano wake na nyota Mr Blue ukatoweka maana alishindwa tena kukaa kileleni hivyo kutajwa tajwa.

Kwa wasiofahamu, Joslin alijikuta akiimba wimbo mmoja na hasimu wake wa wakati huo, Mr Blue, wimbo wa Dully Sykes, uliojulikana kama 'Dhahabu'. Vijana hawa walifunikana balaa. Inadaiwa kuwa hakuna aliyejua kuwa anaimba wimbo mmoja na mwenzake.

Kila mmoja aliingiza sauti kwa wakati wake. Baadaye ukawa wimbo matata sana katika anga ya muziki wa BONGO FLEVA. Je, nani anajua msanii huyu anafanya nini kwa sasa?

Amepotea kabisa. Blog yako ya Handeni imemkumbuka kijana na inajaribu kuelezea namna alivyoweza kuimba kwa ustadi wa aina yake. Hapana shaka baada ya kuandika haya kijana huyu ataibuka na kuelezea wapi yupo, anafanya nini na kwanini ameanguka?

Alikuwa msanii mkali sana. Ana kipaji cha aina yake.
Huyu ndio msanii anayekumbukwa kwa leo.
Wiki ijayo tutaendelea na kumkumbuka nyota mwingine wa sanaa na kuelezea kazi zake ambapo hata hivyo alionekana kutoweka.

Unamkumbuka msanii gani, wakati huo wewe unafanya nini?

Tutajie au muelezee kisha tutumie kwa email yetu kambimbwana@yahoo.com au +255712053949


SIWEZI KUVUMILIA: Nani mkweli, sakata la Okwi?

$
0
0

Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

SI lengo langu kuchokoza moto uliozima, baada ya kudaiwa kuwa Shirikisho la Mpira wa Miguu duniani (FIFA), limebariki mshambuliaji kutoka Uganda, Emmanuel Okwi kukipiga katika timu ya Yanga, ikiwa ni uamuzi uliochukuliwa baada ya kuombwa na Shirikisho  la Soka nchini (TFF), kutokana na mkanganyiko uliobuka.
Emmanuel Okwi, mshambuliaji wa Kimataifa wa Yanga.
Hii ni kwasababu ninaamini kuwa ili mchezaji afikie malengo yake lazima avae jezi na kushiriki katika mechi za ndani na nje ya nchi, hasa kama timu yake inashiriki kimataifa.


Kwa mchezaji mwenye malengo, ni lazima atake kucheza Yanga na Azam FC maana kwa mwaka huu ndio zinazoshiriki michuano mikubwa Afrika, ukiacha mechi za ligi ya nyumbani.


Tangu asajiliwe na Yanga katika usajili wa dirisha dogo, Okwi aliingia kwenye mzozo baada ya usajili wake kuzuiwa kwa madai kuwa ulikuwa na utata.


Ni kweli ulikuwa na utata. Na hata sasa utata huo bado ni utata maana unaumiza kwa zamu. Katika kuliangalia jambo hilo, ni wazi Dunia ya leo si ya ubabaishaji.


Klabu za Yanga, Simba na nyinginezo zinapaswa kusajili kwa kufuata taratibu zote. Hali kazalka kwa wasimamizi wa soka, likiwamo Shirikisho la Soka nchini (TFF), Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) na wadau wengine lazima wasimame imara.

Kinyume cha hapo siwezi kuvumilia. Ingawa napenda Okwi aiwakilishe Yanga katika ligi ya Tanzania Bara na Ligi ya Mabingwa Afrika, ila ubabaishaji huu hauna tija.


Kuruhusiwa kucheza kwa Okwi ndani ya Yanga ni jambo zuri mno kwa wadau wa timu hiyo. Lakini pia iwe sababu ya kuhoji nani mkweli kwenye sakata hili. Etoile Du Sahel waliyompata Okwi kwa klabu ya Simba, Yanga iliyomnunua au SC Villa ya Uganda, ambazo zote zinalilia haki ya mchezaji huyo.


Kuna siku kutatolewa uamuzi mgumu utakaosababisha hasara kwa timu na Taifa kwa ujumla. Miongoni mwa hasara hizo ni kupokwa ushindi uliopatikana kwa tabu uwanjani.


Kwa bahati mbaya FIFA wamekuwa makini sana katika kusimamia kanuni na taratibu zao zinazoendesha soka. Inapotokea uzembe na ubabaishaji ni rahisi kuchukua hatua.


Hili likichukuliwa kwa timu za Tanzania, ikiwamo Yanga au Simba, malalamiko yake hayataelezeka. Huu ndio ukweli, hivyo wakati huu mashabiki wa Yanga wanafurahia Okwi kukipiga Yanga, ni wakati wa kujiuliza nani mkweli?


Tukishajua mkweli ni nani, tusimamie vyema sheria ili kesho zikichukuliwa juu yetu isiwe na madhara. Tusilalamike, ukizingatia kuwa sisi ni mabingwa wa kulalama kuhujumiwa.


Kinyume cha hapo matukio mfano wa Okwi yataendelea kutokea na kuibua mzozo usiokuwa na kichwa wala miguu, maana tumeamua kuwa watu wa kubabaisha.

Tukutane tena wiki ijayo.


+255 712053949

Edward Lowassa, Bernard Membe kitanzini CCM

$
0
0

KAMATI YA MAADILI CCM
TAARIFA RASMI YA CCMKati ya tarehe 13/02/2014 na tarehe 18/02/2014 kumekuwa na mfululizo wa vikao kadhaa vya Chama kitaifa vilivyoshughulikia suala la maadili ndani ya Chama.
Vikao hivyo ni pamoja na Kamati Ndogo ya Udhibiti tarehe 13-14/02/2014, Tume ya Udhibiti na Nidhamu 18/02/2014 na Kamati Kuu tarehe 18/02/2013.
Waliohojiwa katika mfululizo wa vikao hivi ni wafuatao:-
1. Ndgugu Frederick Sumaye2. Ndugu Edward Lowasa3. Ndugu Bernard Membe 4. Ndugu Stephen Wassira5. Ndugu January Makamba 6. Ndugu William Ngeleja
Baada ya kuwahoji ilithibitika kuwa baadhi ya tuhuma dhidi yao ni za kweli na hivyo kupendekeza adhabu. Mapendekezo hayo yalipelekwa kwenye Tume ya Udhibiti na Nidhamu na hatimaye Kamati Kuu ya CCM ambayo ilitoa adhabu kwa wahusika.
Kwa ujumla waliohojiwa wamethibitika kuwa na makosa yafuatayo:-
1. Walithibitika kuanza kampeni za kutafuta kuteuliwa kugombea Urais kabla ya wakati kinyume na Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM Toleo la Februari 2010, Ibara 6(7)(i).
2. Wamethibitika kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya Chama na baadhi yao kufanya vitendo vinavyokiuka maadili ndani ya jamii. Kosa hili nalo ni kwa mujibu wa Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM Toleo la Februari 2010, Ibara kadhaa za kanuni hizo.
Kamati Kuu baada ya kuthibitisha makosa hayo imewapa watu wote sita waliohojiwa adhabu ya ONYO KALI na kuwataka wajiepushe na vitendo vinavyokiuka maadili na iwapo wataendelea na vitendo hivyo Chama kitawachukulia hatua kali zaidi.
Tafsiri ya adhabu ya ONYO KALI kwa mujibu wa Kanuni za Uongozi na Maadili za CCM Toleo la Februari 2010, Ibara ya 8(ii) (b) ni:-
“Mwanachama aliyepewa adhabu ya ONYO KALI atakuwa katika hali ya kuchunguzwa kwa muda usiopungua miezi 12, ili kumsaidia katika jitihada zake za kujirekebisha.”
Kamati Kuu imeitaka pia Kamati Ndogo ya Udhibiti kuwachunguza na kuchukua hatua kwa wote waliohusika kwa namna moja au nyingine (mawakala na wapambe) kufanyika kwa vitendo hivyo vilivyovunja Kanuni za Chama.
Aidha, Kamati Kuu imewaonya vikali Viongozi na Watendaji wa Chama na kuwataka kujiepusha kujihusisha na matendo ya wanawania Urais yanayovunja na kukiuka maadili ya Chama, wametakiwa kuzingatia Kanuni na taratibu za Chama.
Imetolewa na:- Nape Moses Nnauye,KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA TAIFA,ITIKADI NA UENEZI,18/02/2014


Wachoma Nyama wapigwa msasa - Mwanza

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, Mwanza
KAMPUNI ya Bia Tanzania(TBL) kupitia kinywaji chake cha Safari Lager jana imetoa mafunzo kwa  wachoma nyama kutoka Baa mbali mbali za Mkoa wa Mwanza ikiwa ni maandalizi ya mashindano ya Safari Nyama Choma kwa mwaka 2014 yatakayo fanyika katika viwanja vya Furahisha.

Jaji Mkuu wa Safari Lager Nyama Choma, Lawrence Salvi
Akizungumza na waandishi wa habari, Meneja matukio wa Kampuni ya Bia Tanzania(TBL) kanda ya Ziwa, Erick Mwayela, alisema lengo la kutoa mafunzo ni kutoa elimu kwa wachoma nyama ukizingatia uchomaji nyama ni moja  sehemu ya kujiingizia kipato katika Bar. 

Mwayela alisema kutokana na hali hiyo wakaona ni vema wakaendesha Semina kwa wachoma nyama ili waweze kukidhi vigezo vya mahitaji ya Wateja ili waweze kufurahia Nyama choma kama ilivyo kwa vyakula vingine ili kuendana na kauli Mbiu ya Bia ya Safari Lager isemayo“ Safari Lager bila nyama choma haijakamilika.”

Aliongeza kuwa baada ya mafunzo hayo yaliyotolewa kwa Baa 37 ambao wametunukiwa vyeti vya ushiriki  pia kutakuwa na mashindano ya kuchoma nyama ambapo washindi 10 watapatikana kutokana na watakaofuzu vigezo na masharti waliyopewa katika semina hiyo.

Alisema Fainali za Mashindano zitafanyika Machi 9, Mwaka huu katika Viwanja vya Furahisha ambapo washindi watapewa zawadi kuanzia mshindi wa kwanza atakayejinyakulia Shilingi Milioni moja na Kikombe, mshindi wa pili Laki nane, Mshindi wa tatu Laki 6, Mshindi wa nne laki nne na Mshindi wa Tano shilingi laki mbili huku mshindi wa Sita hadi wa Kumi watajinyakulia kifuta jasho cha shilingi 50,000/=.

Alisema namna ya kuwapata washindi ni kutokana na wateja kupiga kura katika utaratibu utakaobandikwa katika Baa shiriki ambapo mteja atapiga kura kupitia simu ya mkononi ili kuichagua baa inayochoma nyama vizuri.

Aliongeza kuwa baada ya zoezi hilo kukamilika katika Mkoa wa Mwanza itaendelea katika Mikoa mingine ambayo ni Kilimanjaro,Arusha na Dar Es Salaam, mikoa ambayo imetajwa kuwa ndiyo vinara wa uchomaji nyama pamoja na kuongoza kwa mauzo ya bia ya Safari Lager tofauti na maeneo mengine.

Kwa upande wake Mkufunzi wa Mafunzo hayo, Laurence  Salvi ambaye pia ni Jaji Mkuu wa mashindano hayo amesema huwezi kuandaa mashindano bila ya kutoa Elimu, hivyo TBL wamefikiria jambo la msingi sana lenye manufaa kwa waandaaji yaani wachoma nyama mpaka kwa watumiani yaani mlaji.
Bwana Lawrence binfsi aliishukuru TBL kupitia bia ya Safari Lager kufikiria jambo zuri la kufadhili elimu kwa kwa wachoma nyama jambo ambalo si faida kwa wachoma nyama tu bali hata watumiaji sasa watakula nyama inayostahili.

Tunasubiria matokeo ya mkutano wa wadau wa masumbwi

$
0
0
Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam

HIVI karibuni wadau wa mchezo wa masumbwi walifanya mkutano wa kujadili tasnia hiyo inayokabiriwa na changamoto nyingi, hasa kwa kuona kampuni zinavyouchunia mchezo huo.


Ingawa wamekalia pesa lukuki, lakini wadau hao wameendelea kuziba macho na masikio yao, hata pale tunapoona malalamiko ya wadau wa ngumi na mabondia kuwa wanakosa udhamini.

Bondia Francis Cheka, pichani.
Changamoto hizo ndio sababu inayoufanya mchezo huo ushindwe kupiga hatua kubwa, jambo lililowafanya wadau hao wakutane katika mkutano wao uliofanyika katika Ukumbi wa Vijana Social Hall, Kinondoni, jijini Dar es Salaam.


Waswahili wanasema kupanga ni kuchagua. Kwakuwa wadau hao wameamua kupanga jinsi ya kukabiriana na changamoto hizo, basi ni jambo jema kwao.


Hata hivyo, wadau hao wanakutana kwenye kikao chao wakati wao wenyewe wakati mwingine hawapo makini. Kwa mfano, mwishoni mwa mwaka jana kulikuwa na kadhia kubwa.


Ni pale promota wa mchezo wa masumbwi, Jay Msangi alivyoutia aibu kwa kuandaa pambano la Kimataifa kati ya Francis Cheka na Mmarekani, Phil Williams.


Ingawa pambano hili la Ubingwa wa Dunia lilimalizika kwa Cheka kushinda na kulitangaza Taifa, ila kasumba ni pale promota alivyoshindwa kujipanga katika suala zima la malipo.

Awali mpambano huo ulitaka kushindwa kufanyika, hivyo serikali kuingilia kati kunusuru zogo hilo, ambalo hadi mwisho ingekuwa aibu kwa Tanzania nzima.


Si nia yangu kukumbushia kilichotokea mwezi Agosti mwaka jana, ila ni namna gani wadau wa ngumi wote wanapaswa kufanyia kazi majibu ya mkutano wao.


Huu ndio ukweli. Wadau hao wakiamua kufanyia kazi yale waliyoamua wenyewe kwa ajili ya kunusuru tasnia hii itakuwa ni jambo la busara kwao na manufaa ya mchezo wa ngumi.


Huu ni wakati wa kufanya jitihada za kuukomboa mchezo wa masumbwi. Kila mtu mwenye malengo na mchezo wa masumbwi anapaswa kuamua kwa dhati kufanya kila analojua kwa ajili ya maendeleo ya ngumi.


Mapromota mfano wa Msangi nao wanapaswa kubadilika na kuamua kufanya juhudi kujijengea heshima ili walau waaminike katika kuandaa mapambano makubwa zaidi.


Kinyume cha hapo kasumba hii itaendelea. Mchezo wa masumbwi utazidi kudidimia. Wadau wakubwa wote watakimbilia katika michezo mingine, hasa mpira wa miguu.


Matokeo yake ni kuona ngumi inapoteza thamani yake, ingawa kuna vijana wengi wanaoweza kucheza masumbwi kwa ajili ya maisha yao na Tanzania kwa ujumla.


Mabondia wote wenye kiu ya kucheza ngumi watapoteza thamani yao, maana hakuna juhudi za dhati za kuleta ushindani, ukizingatia kuwa juhudi zao ni sifuri.


Hili linapaswa kuangaliwa upya, hasa kwa kuona mkutano wa wadau wa ngumi umekuwa na tija kwa mchezo huo Tanzania, ili kuleta picha na juhudi halisi za kuendeleza ngumi na kuona vijana wengi wanaibuka kwa kasi kushiriki kwenye masumbwi.


+255 712053949

TCRA yakabidhiwa ripoti ya tathmini ya uhamaji wa mfumo wa analojia

$
0
0


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UZIMAJI MITAMBO YA MFUMO WA UTANGAZAJI WA ANALOJIA AWAMU YA PILI
1.0  UTANGULIZI
Mamlaka ya Mawasiliano imepokea matokeo ya tathmini ya zoezi la uhamaji toka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda kidijiti. Zoezi hili lilifanyika kwenye miji saba kama ilivyotajwa kwenye taarifa iliyotolewa na wataalamu wa Chuo kikuu cha Dar e salaam waliofanya tathmini ya Uzimaji wa Mitambo ya Analojia katika Awamu ya Kwanza.
Mkurugenzi wa TCRA, Profesa John, Nkoma, pichani.
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilifanya kamisheni kwa Chuo Kikuu cha Dar es salaam kufanya tathmini ya uzimaji wa Mitambo ya Analojia katika Awamu ya Kwanza, ikitambua kuwa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam kuna wataalamu wenye uzoefu mkubwa wa kufanya tathmini za aina mbalimbali, na kwamba uzoefu huo utasaidia sana kuhakikisha kuwa tunapata taarifa ya uhakika itakayotuwezesha kuboresha zoezi hili kwenye awamu inayofuata.

Nachukua nafasi hii kuwapongeza wataalamu waliohusika katika tathmini hii kwa weledi wao kwenye kazi hii muhimu kwa taifa letu kulingana na matokeo yaliyowasilishwa kitaalamu mbele yenu waandishi wa habari leo hii.

Tanzania ni nchi ya kwanza kuzima mtambo ya analojia Barani Afrika. Uamuzi wa kufanya hivyo, na matokeo yake, umeiletea sifa kubwa nchi yetu kwa jinsi ambavyo Tanzania ilijipanga na kutekeleza maazimio yaliyofikiwa kimataifa kwa wakati na weledi mkubwa. Hii imeonyesha wazi jinsi Serikali ilivyoweza kushirikiana na taasissi zake pamoja na wadau wote katika kutimiza azma hii iliyoafikiwa kimataifa tangu 2006. 
Zoezi la uzimaji mitambo kwa awamu ya kwanza iliyoanza taree 31 disemba 2013 halikuwa rahisi kama wengi wetu tunavyoweza kufikiria, kwani liligusa nyanja nyingi zikiwemo za kijamii, kibiashara, kiufundi na Kisiasa. Mamlaka kama mdhibiti wa sekta ya Mawasiliano, ilibidi kuzingatia matakwa ya nyanja zote na wadau mbalimbali bila kuathiri utoaji wa habari nchini. Inakadiriwa kuwa mpaka kumaliza zoezi hili, mitambo ya kurushia matangazo kwa mfumo wa analojia isiyopungua 60 itakuwa imezimwa. Hali hii imefanya Tanzania kuwa nchi ya pekee na kuifanya nchi yetu kuwa kituo cha mafunzo kwa nchi nyingi ambazo sasa zimekuwa zikifika kujifunza hapa nchini. 

Uamuzi wa kufanya mkutano wa nchi za SADC na ule wa nchii za Jumuiya ya Madola kuhusu Mfumo mpya wa utangazaji wa kidijiti kwa sekta ya utangazaji hapa nchini hivi karibuni, ni matokeo ya mafanikio makubwa tuliyo yapata kwenye zoezi hili lililoendeshwa kitaalamu na Serekali yetu kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).

2.0  UPELEKAJI WA MKONGO WA TAIFA KWENYE VITUO VYA KURUSHIA
MATANGAZO

Mamlaka ya Mawasiliano kwa kushirikiana na Wizara na Kampuni ya Simu ya TTCL tuko kwenye mchakato wa kuhakikisha kuwa vituo vyote vya kurushia matangazo vinafikiwa na mkongo wa Taifa (Optic fiber cable).

Madhumuni ya jitihada hizi, ni kuona kuwa mbali na huduma ya msingi ya kurusha matangazo ya televisheni, vituo vya utangazaji vinatoa huduma za ziada zipatikanazo kwenye mfumo wa kidijiti. Kwa lugha ya kitaalam ni “interactive services”. Napenda kuchukua nafasi hii kuvitaka vituo vya utangazaji vyote nchini kuwa wabunifu na kutumia fursa zilizopo kwenye teknolojia hii ya kidijiti ili wananchi waweze kuona tofauti kubwa kati ya mfumo wa zamani wa analojia na huu mpya wa kidijiti.

3.0   UZIMAJI MITAMBO YA ANALOJIA AWAMU YA PILI
Baada ya kupokea matokeo ya tathmini Awamu ya Kwanza, Mamlaka ya Mawasiliano inajipanga kuzima mitambo kwa awamu ya pili na ya mwisho. Katika awamu hii, inategemewa miji 12 itahusika na uzimaji wa mitambo ya analoja. Lakini kama maafikiano yalivyofanyika awali, uzimaji utafanyika tu pale ambapo huduma za utangazaji wa kidijiti umefika.  Vigezo vyote vitano tulivyokubaliana na wadau vitahakikishwa kuwa vinatimizwa kabla ya kuzima mitambo hiyo.

Ni matarajio ya Mamlaka kuwa wasimikaji wa mitambo ya kidijiti (Multiplex Operators) wataendelea kwa kasi ufungaji wa mitambo hiyo hasa kwenye maeneo ambayo mfumo wa analojia unatumika. Mpaka sasa miji mingine 7 inapata huduma ya matangazo ya kidijiti nayo ni Morogoro, Singida, Tabora, Musoma, Kigoma, Bukoba na Kahama. Mchakato wa kufunga mitambo ya kidijiti kwenye miji iliyobaki inaendelea vizuri. Tunatarajia kuwa vituo vya utangazaji vitatoa ushirikiano mkubwa kama ule tulioupata kwenye awamu ya kwanza.

 Mamlaka imeyachukua mapendekezo yote yaliyotolewa kwenye ripoti hii na tunaahidi kuwa tutayafanyia kazi. Yale yaliyo nje ya uwezo wetu tutayafikisha mahali panapohusika kwa utekelezaji zaidi.

Mwisho, napenda kuwafahamisha kuwa Mamlaka imependekeza rasimu ya ratiba ya uzimaji mitambo awamu ya pili na ya mwisho itakayotangazwa na Waziri mwenye dhamana ya sekta ya Mawasiliano hivi karibuni. 

Katika mapendekezo ya Mamlaka, tunakusudia kuanza awamu ya pili katika miji ya Singida na Tabora mnamo mwishoni wa mwezi Machi 2014. Miji mingine katika awamu ya pili itakuwa Musoma, Bukoba, Morogoro, Kahama, Iringa, Songea na Lindi. Awamu ya pili inategemewa kukamilika mwishoni mwa mwezi Oktoba 2014.

Nia ya Mamlaka ni kuona zoezi hili la uhamaji kutoka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda mfumo wa kidijiti linakamilka katika nchi yetu kabla ya kufikia ukomo wa matangazo ya analojia kama ilivyoelekezwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalosimamia Mawasiliano Duniani (ITU) siku ya tarehe 17 Juni 2015.


Imetolewa na:
MKURUGENZI MKUU
MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA
19 February 2014

Ripoti kamili iliyokabidhiwa TCRA leo ipitie hatua kwa hatua

$
0
0


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

MAMLAKA YA MAWASILIANO TANZANIA


MATOKEO YA TATHMINI YA MCHAKATO WA UHAMAJI KUTOKA MFUMO WA UTANAGAZAJI WA ANALOJIA KWENDA KIDIJITI


1.0        UTANGULIZI

Mnamo mwezi Julai, 2013, Serikali kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) ilikamisheni jopo la wataalamu wa Chuo Kikuu kufanya tathmini ya mchakato mzima wa uhamaji toka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda mfumo wa kidijiti pamoja na uzimaji wa mitambo hiyo kwenye miji saba ambayo ni Dar e salaam, Tanga, Moshi, Mwanza, Dodoma, Arusha na Mbeya. Uzimaji wa mitambo ya analojia ilikuwa ni kwa mujibu wa sheria, ambayo iko kwenye kanuni zinazojulikana kama “Digital Broadcasting and Other Networks 2011”

Jopo hilo lilijumuisha wataalamu wafuatao:-

Prof. Nerey Mvungi         Mtaalamu wa Mawasiliano ya ki electronic
Dr.Francis Sichona         Mtaalamu wa Takwimu
Mr.F.M Ishengoma        Mtaalamu wa Habari na Mawasiliano

Wote hawa ni wafanayakazi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.


1.1                MADHUMUNI YA TATHMINI
Madhumuni ya tahmini hii ilikuwa imejengwa kwenye maeneo Makuu manne kama ifuatavyo;

(a)  Tathmini ya utendaji na utoaji huduma za utangazaji kwenye mfumo wa kidijiti ikiwa ni pamoja na usimikaji wa miundo mbinu ya kidijiti.

(b)Tathmini ya kuangalia jinsi Mamlaka ya Mawasiliano ilivyokuwa imejizatiti kuandaa na kusimamia zoezi zima la uhamaji toka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda kidijiti

(c)  Tathmini ya jinsi watumiaji wa huduma za utangazaji walivyopokea mabadiliko hayo na changamoto zilizopo na

(d)Tathmini ya jinsi zoezi zima la uzimaji mitambo lilivyoendeshwa.

Katika uendeshaji wa tathmini hiyo wataalamu walizingatia mambo muhimu yafuatayo ikiwa ni pamoja na hoja zilizotolewa na taasisi na watu mbalimbali kutoka kwenye jamii kama ifuatavyo:-

(i)     Idadi ya visimbuzi vilivyokuwepo kwenye soko kabla ya uzimaji mitambo kama vinatosheleza mahitaji,

(ii)    Idadi ya watu walioweza kununua visimbuzi ilikuwa ndogo hivyo watu wengi kushindwa kununua na kukosa habari zinazopatikana kwa njia ya luninga,

(iii)  Ushirikishaji wa wadau kwenye mchakato mzima wa uhamaji toka mfumo wa analojia kwenda kidijiti kabla ya uzimaji mitambo hiyo,

(iv)  Kiwango cha Elimu kwa Umma (Public Awareness Campaign) kilichotolewa kabla na baada ya uzimaji mitambo,

(v)    Bei za visimbuzi kama zilikuwa juu kwa watu wa hali ya kawaida na kusababisha kushindwa kuvinunua,

(vi)  Ubora wa visimbuzi na upokeaji wa matangazo usioridhisha kama vile kuganda kwa picha.

 
1.2                NJIA ILIYOTUMIKA KUFANYA TATHMINI
Njia iliyotumika kufanya tathmini hii ni ile inayotumika kimataifa (International Best Practise) kuendesha mazoezi kama haya ijulikanayo kama “Sampling Approach” ambapo takwimu hukusanywa kwa kuzingatia uwiano wa kaya zilizopo kwenye eneo husika, jinsia, umri, elimu na kazi za kumuingizia kipato mtu anayehojiwa.

Makundi mabalimbali yanayohusika kwenye mchakato huu wa uhamaji kutoka mfumo wa analojia kwenda dijitali yalihojiwa kwa kupitia dodoso maalumu lililoandaliwa na maoni yao yalikusanywa. Makundi hayo ni kama ifuatavyo:-
(i)           Watumiaji wa huduma ya matangazo kwa mfumo wa kidijiti (Consumers)

(ii)          Watengenezaji na wasambazaji wa maudhui kwa njia ya Luninga (Content Service Providers)

(iii)        Wasimikaji wa miundo mbinu ya kidijiti (Multiplex Operators) na

(iv)        Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania.

2.0        MATOKEO YA TATHMINI
Yafuatayo ni matokeo ya zoezi zima la tathmini hiyo kama ilivyoendeshwa kwenye maeneo tajwa hapo juu.

2.1         TATHMINI YA UTENDAJI NA UTOAJI HUDUMA ZA UTANGAZAJI KWENYE MFUMO WA KIDIJITI IKIWA NI PAMOJA NA USIMIKAJI WA MIUNDO MBINU YA KIDIJTI.
Tathmini iliyoendeshwa na jopo la wataalam kuhusu utendaji na huduma kwa walaji kwa ujumla wake zimeonyesha yafuatayo;

(a)   Asilimia 89% ya kaya za watumiaji (consumers) walikuwa wakitumia huduma ya matangazo kwa mfumo wa kidijiti mara baada ya uzimaji wa mitambo ya analojia kwenye miji saba ambayo tathmini ilikuwa ikifanyika

(b)   Asilimia 11% ya kaya za watumiaji hawakuweza kupokea matangazo ya kidijiti kwa sababu mbalimbali kama ifuatavyo:-

-       5.5% hawakununua visimbuizi

-       0.1% ya Kaya, walisema visimbuzi vilikuwa havipatikani

-    3.2% ya Kaya, walishindwa kunua visimbuzi sababu ya bei kuwa juu

-       0.2% ya Kaya visimbuzi vyao vilikuwa vibovu

-     0.3% ya Kaya, visimbuzi havikuweza kupokea matangazo ya kidijiti kwa sababu ya mawimbi hayapatikani kwa ubora zaidi (Poor signal reception)

-       0.9% ya Kaya Luninga (TV screen) zilikuwa mbovu

-       0.7% ya Kaya hawakuwa na umeme
2.2        UTAYARI WA MAMLAKA YA MAWASILIANO KUANDAA NA KUSIMAMIA ZOEZI ZIMA LA UHAMAJI TOKA UTANGAZAJI WA MFUMO WA ANALOJIA KWENDA KIDIJITI

Jopo la wataalamu lililokuwa likiendesha tathmini hii liliweza kuthibitisha kuwepo kwa mambo yafuatayo pamoja na baadhi ya nyaraka kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA):-

-       Kuwepo kwa kamati ya Kiufundi inayoundwa na wadau mbalimbali ikiwa na kazi ya kutoa ushauri wa kiufundi kwa maswala yote yanayohusu uhamaji toka utangazaji wa analojia kweda kidijiti,

-       Kuwepo kwa dira madhubuti inayoonyesha mambo muhimu ya kutekelezwa kuelekea uzimaji wa mitambo ya analojia,

-       Kuwepo kwa sheria na kanuni zinazosimamia zoezi la uhamaji toka analoja kwenda kidijiti,

-       Kuwepo kwa nyaraka mbalimbali zinazoonyesha muhtasari wa vikao mbalimbali vilivyofanywa kati ya wadau na Mamlaka ya Mawasiliano.

              Vilevile Jopo la wataalamu liliweza kuthibitisha mambo yafuatayo:-

-    Muundo bora wa leseni unaozingatia utoaji huduma za matangazo ya kidijiti,

-    Utaratibu mzuri wa ushindani kwa njia ya wazi uliotumika kuwapata “Multiplex Operators” (wajenga Miundombinu na Wsambazaji wa matangazo),

-     Waraka unaonyesha mchakato wa namna ya kupata malipo yananayotakiwa kulipwa na watengenezaji na wasambazaji wa  maudhui (Transmission fee) kwa wenye leseni ya miundo mbinu ya kidijiti (Multiplex Operators),

-    Mfano wa nyaraka itakayotumika kufikia makubaliano ya utoaji huduma na mahusiano yao kibiashara (SLA) kati ya wasimikaji wa miundo mbinu ya kidijiti na watengenezaji na wasambazaji maudhui.

Kutokana na vielelezo na nyaraka ambazo jopo la wataalamu iliweza kuzipata, jopo limeridhika kabisa kuwa Mamlaka ya Mawasiliano ilikuwa imejizatiti vizuri kuandaa na kusimamia utekelezaji wa uhamaji toka mfumo wa zamani wa analojia kwenda utangazaji wa mfumo mpya wa kidijiti.

2.3          MATOKEO YA TATHMINI KUHUSU UPATIKANAJI WA VISIMBUZI NA ELIMU KWA UMMA

Tathmini imeonyesha kuwa kati ya kaya zote zilizohojiwa kwenye miji saba, ni 0.1% ya kaya zilizodai uhaba wa visimbuzi wakati wa zoezi zima la uzimaji mitambo ya analojia. Matokeo mingine ni kama ifuatavyo:-

-     35.4% ya kaya zilizohojiwa walinunua visimbuzi kabla ya uzimaji mitambo ya analojia na kabla ya kuanza utoaji wa elimu kwa umma kuhusu mfumo mpya wa uatangazaji wa kidijiti

-    29.5% ya kaya walinunua visimbuzi kabla ya uzimaji mitambo ya analojia lakini baada ya utoaji elimu kwa umma

-       35.1% walinunua visimbuzi baada ya uzimaji mitambo
          Takwimu hizi zinaonyesha kuwa upatikanaji wa visimbuzi na bei halikuwa   tatizo kubwa lililoathiri mchakato mzima wa uhamaji kutoka mfumo wa      analojia kwenda kidijiti kwenye miji hii saba. Vilevile elimu kwa umma ilisaidia sana kuhamasisha walaji kuhamia kwenye mfumo huu mpya wa utangazaji


2.4           ZOEZI LA UZIMAJI MITAMBO YA ANALOJIA
Ilifahamika kuwa zoezi la uzimaji mitambo ya analojia lilifanyika kwenye awamu nne ambapo kila awamu ilitoa nafasi ya mwezi mmoja. Jopo la wataalam limeridhika na utaratibu huu, ambao unatoa nafasi kubwa ya kutathmini matatizo yanayojitokeza kwenye awamu ya kwanza kabla ya kwenda kwenye awamu nyingine. Vilevile ulitoa fursa ya kuhakikisha kuwa eneo linalofuata linakuwa na visimbuzi vya kutosha na elimu kwa umma inatolewa kikamilifu kwa kutumia Radio na Televissheni za eneo husika.


2.5          WATENGENEZAJI NA WASAMBAZAJI MAUDHUI (CONTENT SERVICE PROVIDERS)
65% ya watengenezaji na wasambazaji wa maudhui walikuwa wamejiunga na mfumo wa kidijiti kabla ya uzimaji wa mitambo ya analojia.
Sababu kubwa ya vituo vingine kutojiunga na mfumo huu kwa wakati ilikuwa ni sababu za kimazoea kwamba huenda mitambo isingezimwa kwa wakati uliopangwa.

Mpaka sasa vituo vyote vilivyopo Dar es Salaam vimeshajiunga na mfumo huu kasoro kituo kimoja.


3.0        MAJUMUISHO

3.1       Jopo la wataalam limeridhika kuwa watazamaji wengi waliokuwa kwenye mfumo wa analojia walijiunga kwenye mfumo wa kidijiti. 11% tu ndio ambao hawakuweza kujiunga kwa sababu mbalimbali kama nilizoelezea mwanzoni. Idadi hiyo inaweza kuwa imepungua kwa vile watu wamekua wakiendelea kununua visimbuzi,

3.2       Zoezi hili halijawanyima watanzania haki ya kupata habari kwani wengi tayari wameshajiunga na mfumo huu mpya. Jopo liliona kuwa sababu ya malalamiko mengi yalitokana na tabia halisi ya wanadamu kuogopa mabadiliko,

3.3       Kutokana na takwimu zilizokusanywa, jopo limeridhika kabisa kuwa elimu kwa umma ilitolewa kwa kiwango kikubwa kwani 90% ya kaya zilizotembelewa walikuwa na habari kuhusu mfumo huu mpya wa utangazaji kwa njia ya kidijiti,

3.4       Hatua madhubuti zilichukuliwa kuhakikisha kuwa kabla eneo husika kuzimwa mitambo ya analojia kulikuwa na visimbuzi vya kutosha,

3.5       Mfumo huu mpya wa kidijiti utatoa fursa nzuri kwa watengenezaji na wasambazaji wa maudhui kutumia muda wote kutengeneza vipindi vizuri badala ya kujihusisha na usimikaji miundo mbinu ya utangazaji,

3.6       Mfumo huu mpya wa utanagazaji kwa njia ya kidijiti umeongeza ubora wa picha na channel nyingi. Juhudi zifanyike kuwa na channel nyingi za nyumbani badala ya nje ya nchi.

3.7       Jopo limeridhika kuwa mfumo huu mpya haujapunguza idadi ya watazamaji wa luninga ila watazamaji wamegawanyika kutazama channel mbalimbali na hivyo kujenga hisia kuwa watazamaji wamepungua.

3.8       Maeneo mengi yaliyokuwa yanapokea channel moja mpaka tatu sasa wanaweza kuona channel za kinyumbani zaidi ya tano.

3.9       Uhamaji kutoka DVB-T kwenda DVB-T2 uende kwa nguvu ya soko kwani dhana nzima ilikuwa kuhama mfumo wa analojia kwenda kidijiti, na viwango vyote hivi viwili vinatoa matanagazo ya kidjiti


4.0        HITIMISHO

Kutokana na matokeo ya tathmini iliyofanyika serikali inashauriwa iendelee na zoezi la uzimaji mitambo ya analojia sehemu zilizobakia. Jopo limeridhika na uandaaaji na usimamizi wa zoezi hili na kwamba kasoro zilizojitokeza ni sababu ya hofu ya mabadiliko na uzoefu wa walaji kwenye matumizi ya visimbuzi. Vilevile kuna faida nyingi za mfumo wa kidijiti ambazo watoa huduma wanatakiwa kuzitumia ili kuchochea ukuaji wa uchumi nchini.

Serikali inashauriwa kutoa punguzo la kodi kwa visimbuzi ili kuwawezesha watanzania wengi zaidi kununua visimbuzi na kupata habari kwa njia ya Luninga

Naomba niwakabidhi ripoti hii ambayo ina maelezo na taarifa za kina kuhusu zoezi tathmini hii.



Imetolewa na:


Prof. Nerey Mvungi        Mtaalamu wa Mawasiliano ya ki electronic
Dr.Francis Sichona         Mtaalamu wa Takwimu
Mr.F.M Ishengoma        Mtaalamu wa Habari na Mawasiliano

JOPO LA WATAALAMU TOKA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM
19 FEBRUARI 2014

Mkuu wa Mkoa Tanga awashauri wanafunzi kuzingatia masomo yao na kuacha kufikiria ngono

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Chiku Gallawa, pichani.
Na Oscar Assenga, Muheza
MKUU wa Mkoa wa Tanga, Luteni Mstaafu, Chiku Gallawa amewataka wanafunziwa shule za msingi na sekondari wilayani hapa kuacha kujiingiza kwenye mapenzi wakiwa mashuleni kwani hali hiyo itawafanya kushindwa kufikia malengo yao.
 
Gallawa alitoa kauli hiyo  wakati akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari ya Potwe kwenye ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo,kusikiliza kero za wanannchi kupitia mikutano ya hadhara kwenye kata na vijiji mbalimbali wilayani hapa.
 
Alisema wanapaswa kutumia vizuri muda wao wakiwa shuleni kwa kujisomea kwa bidii ikiwemo kupenda masomo ya sayansi ili waweze kuongeza kasi ya wataalamu wa masomo hayo kwa siku zijazo kitendo ambacho kitaongeza hamasa ya wenzao wengine.


"Hakikisheni mnatumia vizuri muda wenu kwa kusoma kwa bidii kwanihiyo ndio silaha pekee ambazo itawainua kimaisha na kuwakwamua naumaskini walionao kwenye jamii zenu na Taifa kwa ujumla ikiwemo kuachakujiingiza kwenye mapenzi," alisema.
 
Akizungumzia suala la upandaji wa miti,Mkuu huyo wa mkoa aliagizavitalu vya miti kwa shule za msingi na sekondari kuhakikisha wanapandamiti ipatayo 4000 ili kusaidia kuepukana na ukosefu wa mvua na uharibifu unaosababishwa na upepo mkali.
 
Awali akizungumza kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Tanga,Mkuu wawilaya ya Muheza,Subira Mgalu alisema wilaya hiyo imeanzisha msakomaalumu wa kusaka wazazi ambao hawajawapeleka watoto wao shuleniwaliofaulu.
 
Mgalu alisema ikibainika wanafunzi hao wameozeshwa wazazi watachukuliwa hatua kali ikiwmo kufikishwa kwenye vyombo vya sheriaili kuweza kukomesha vitendo vya aina hiyo wilayani humo.      

"Mh.Mkuu wa Mkoa Tumeweka utaratibu wa kutoza faini ya sh.elfumoja kwa wanafunzi watoro ambapo fedha hizo huhesabiwa kwa kila sikualiokosa na hupelekwa kwenye uchangiaji wa ujenzi wa maabara "AlisemaDC Mgalu.

Jeshi la Polisi Singida lakamata meno ya tembo ya Sh Milioni 17

$
0
0
Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Singida, SSP. Cordula Lyimo, akitoa taarifa kwa waandishi wa habari leo juu ya kukamtwa kwa meno ya Tembo vipande 16 vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 17 milioni.Vipande hivyo vimekamatwa februari 16 mwaka huu saa tano usiku kwenye kizuizi cha mazao cha kijiji cha Ukimbu wilaya ya Manyoni. Siku nne zilizopita,vipande vingine 21 vya meno ya Tembo vyenye thamani ya shilingi 43 milioni,vilikamatwa eneo hilo hilo.(Picha na Nathaniel Limu).
Na Nathaniel Limu, Singida
JESHI la Polisi mkoa wa Singida limefanikiwa kukamata vipande 16 vya meno ya ndovu vyenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 17.
Meno hayo yamekamatwa siku nne (12/2/2014) toka meno mengine vipande 21 vyenye thamani ya zaidi ya shilingi 43 milioni, kukamatwa kwenye eneo lile lile la kizuizi cha mazao kilichopo katika kijiji cha Ukimbu kata ya Mgandu wilaya ya Manyoni.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Singida.SSP.Cordula Lyimo amesema meno hayo yamekamatwa febr.16 saa tano usiku huko katika kizuizi cha mazao kilichopo katika kijiji cha Ukimbu,kata ya Mgandu tarafa ya Itigi wilaya ya Manyoni.
Alisema askari wakiwa katika kizuizi hicho,walifanya ukaguzi kwenye gari T.288 AJF aina ya scania mali ya kampuni ya super service likiendeshwa na dereva Ally Hamadi, likitokea Makogorosi Chunya,likielekea Itigi wilaya ya Manyoni.
“Baada ya upekuzi huo,walikuta meno hayo yakiwa yamehifadhiwa ndani ya begi la nguo na kuwekwa kwenye keria za ndani ya basi.Mtuhumiwa aliweza kupatikana wakati akiwa katika juhudi za kutaka kutoka nda ya basi ili akimbie”,amesema Lyimo.
Kaimu kamanda huyo,amesema uchuguzi zaidi unaendelea ili kubaini au kupata mtandao kamili unaojihusisha na kuwinda pamoja na kununua nyara hizo.

Bernard Membe: Amani ya Tanzania sio kigezo cha watu wa nje kutaka kuchafua Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

$
0
0
TAARIFA YA MHE. BERNARD K. MEMBE (MB.), WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA ATAKAYOITOA KWENYE MKUTANO NA WAANDISHI WA HABARI UTAKAOFANYIKA IDARA YA HABARI (MAELEZO) TAREHE 20 FEBRUARI, 2014.

1. KUCHAGULIWA TENA KWA TANZANIA KWENYE BARAZA LA AMANI NA USALAMA LA UMOJA WA AFRIKA (AU)
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, pichani.

Tanzania imechaguliwa kwa mara ya pili mfululizo kuwa Mjumbe wa Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika (PSC) kwa kipindi cha miaka miwili kuanzia mwaka huu. Tanzania ilichaguliwa kwa mara ya kwanza katika Baraza hilo mwaka 2012.


Miongoni mwa sababu muhimu zilizopelekea Tanzania kuchaguliwa kwa mara nyingine kwenye Baraza la Amani na Usalama la Umoja wa Afrika ni pamoja na:-

a. Heshima iliyojijengea kimataifa, hususan katika utatuzi wa migogoro ya kikanda kama ile ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na Madagascar;

b. Tanzania imekuwa mstari wa mbele kuchangia vikosi vya kulinda amani kwenye maeneo mbalimbali yenye migogoro kama vile Darfur, DRC, Lebanon n.k;

c. Kuaminika kwa vikosi vya Tanzania vinapopelekwa kulinda amani kwa sababu ya ujuzi, nidhamu na kujituma.


TANZANIA YAJIJENGEA HESHIMA

Mbali na kupata fursa adimu ya kushughulikia moja kwa moja masuala nyeti ya amani na usalama Barani Afrika, uanachama wa Baraza la Amani utaijengea Tanzania heshima kubwa hapa Barani na Kimataifa. 


2. VIKOSI VYA KULINDA AMANI KUTOKA TANZANIA

Tanzania imekuwa mstrari wa mbele katika masuala mbalimbali yanayohusu harakati za ukombozi duniani. Tanzania imekuwa pia mstari wa mbele kuchangia vikosi vya kulinda amani kwenye maeneo mbalimbali yenye migogoro Barani Afrika na kwingineko. Hadi sasa Tanzania ina vikosi vya askari huko Lebanon na askari huko Darfur, Sudan. Aidha, Tanzania ilishiriki kikamilifu katika kufikia uamuzi wa kutuma Kikosi cha Kulinda Amani cha SADC nchini DRC. 


Tanzania ilikuwa ni nchi ya kwanza kujitolea kutoa Kikosi Kimoja cha Wanajeshi (Force Intervention Brigade-FIB) huko Mashariki mwa DRC. Wanajeshi kutoka Tanzania ni takriban 1,283 kati ya Wanajeshi 3,069 kutoka Afrika Kusini na Malawi. FIB kwa kushirikiana na vikosi kutoka Afrika Kusini, Majeshi ya Serikali ya DRC na Vikosi vya MONUSCO mwezi Desemba 2014 walifanikiwa kukisambaratisha Kikosi cha Waasi cha M23 na kuwezesha amani Mashariki mwa Kongo kurejea tena.


3. MGOGORO WA TANZANIA NA MALAWI KUHUSU MPAKA KWENYE ZIWA NYASA



Mgororo huu kwa sasa uko chini ya usuluhishi wa Mhe. Joachim Chissano, Mwenyekiti wa Jopo la Usuluhishi wa Jukwaa la Viongozi Wastaafu wa Afrika Ukanda wa SADC.

Mnamo tarehe 27 Novemba, 2013 Tanzania na Malawi ziliwasilisha utetezi wa hoja zao kwa Mwenyekiti wa Jopo la Usuluhishi ilikuliwezesha Jopo hilo kutafakari hoja za pande zote mbili na kutoa uamuzi/ushauri wake kuhusu mgogoro huo.


Kwasasa Tanzania na Malawi zinasubiri kuitwa na Jopo hilo ili kwenda kupokea ushauri/uamuzi wa jopo hilo kuhusu mgogoro huo.
Tanzania inapenda kuiomba Malawi kuendelea kutoa ushirikiano hadi hapo suala hili litakapopatiwa ufumbuzi wa kudumu.


4. MGOGORO WA SUDAN KUSINI


Sudani Kusini ilikumbwa na mapigano mkubwa katikati ya Mwezi Desemba 2013 kati ya vikosi vya serikali na waasi, ambao wanamuunga Makamu wa Rais wa zamani Bw. Riek Machar. Mapigano hayo yalizuka baada ya Rais Kiir kumtuhumu Bw. Machar kufanya Jaribio la kupindua Serikali. 


Mapigano hayo yalichukua sura ya ukabila kati ya kabila la Dinka analotoka Rais Kiir na kabila la Nuer ambalo Bw. Machar anatoka. Hadi sasa zaidi ya watu 1000 wameuawa na 700,000 kulazimika kukimbia makazi yao. Umoja wa Afrika kwa kushirikiana na IGAD iliingilia kati na kuanzisha mazungumzo baina ya pande hizo mbilli. 


Kufuatia mazungumzo hayo, tarehe 2013 Januari 2014 pande hizo mbili zilisaini Mkataba wa Kusitisha Mapigano mjini Addis Ababa, baada ya Serikali kukubali kuachia wafuasi 7 kati ya 11 wa Bw. Machar, ambao Serikali ilikuwa ikiwashikilia kwa tuhuma za kupanga Mapinduzi.

Duru ya Pili ya mazungumzo kati ya pande hizo ilianza tarehe 10 Februari, 2014 kwa lengo la kutafuta suluhu ya kudumu ya mgogoro huo. Upande wa waasi bado unasisitiza kuachiliwa kwa wafuasi 4 waliobaki. Aidha, Waasi wanataka majeshi yote ya nje yaliomo nchini humo kuondoka mara moja. 

Wakati mazungumzo hayo yakiendelea, kulikuwepo na taarifa za mapigano ya kushitukiza baina ya Vikosi vya Serikali na Vikundi vya waasi kwenye baadhi ya maeneo ya nchi hiyo. Tarehe 18 Mwezi huu, mapigano mapya yameibuka katika jimbo la Upper Nile ambapo pande zote zinashutumiana kuvunja makubaliano ya kisitisha mapigano. 

Kwa upande wake Vikosi vya Umoja wa Mataiifa (UNMISS), ambavyo mwezi Desemba 2013 idadi yake iliongeka kutoka 7000 hadi 12,500 vimeendelea na jitihada za kuimarisha amani. Tunaomba kuchukua fursa hii, kutaarifu kuwa Tanzania imeahidi kuchangia vikosi vyake kujiunga na jeshi hili la Umoja wa Mataifa lililoko Sudani Kusini. Pamoja na kuchangia vikosi hivyo Tanzania inaomba pande zinazopigana kusitisha mapigano na kuendelea na mazungumzo ili kupata suluhu ya kudumu ya Mgogoro huo.


5. UHUSIANO WA TANZANIA NA RWANDA


Kama itakavyokumbukwa vyombo vingi vya habari viliripoti kudorora kwa uhusiano kati ya Tanzania na Rwanda. Baada ya mazingumzo kati ya Rais Kikwete na Rais Kagame yaliofanyika Mjini Kampala mwezi Septemba, 2013 hali ya uhusiano wetu iliboreka.


Hata hivyo hivi karibuni vyombo ya habari vya Rwanda lilikiwemo Gazeti la Serikali la “News of Rwanda” Vimetoa taarifa za kuishutumu Tanzania na viongozi wake. Aidha kumekuwepo na taarifa za kuishutumu Tanzania kufanya mazungumzo na viongozi wa upinzani nchini Rwanda akiwemo ambapo Waziri Mkuu wa zamani wa Rwanda, Bw Faustine Twagiramungu. 


Serikali ilijibu shutuma hizo kwa kueleza kuwa Tanzania haisaidii vikundi vyovyote vya waasi na pia haijawahi kufanya mazungumzo wala kuwakaribisha viongozi wa Upinzani wa Rwanda.


Historia ya Nchi yetu tangu uhuru inajulikana kuwa tumekuwa tukisisitiza Amani Barani Afrika na hivyo hatuna sababu yoyote wa kusaidia waasi ili kuchochea migogoni. Hivyo, tunaomba kuchukua nafasi hii kuwaonya wale wote wanaotaka kuchafua sifa nzuri ya Tanzania kuacha mara moja. 


Aidha tunawaomba wanahabari kutoshabikia taarifa hizi za uzushi.
Tanzania siku zote inataka uhusiano mzuri na jirani zake lakini tusingependa kupenda Amani kwetu kuwe ndiyo sababu ya watu kutaka kutuchafua. 

6. URAIA WA NCHI MBILI (DUAL CITIZENSHIP) UTAMBULIWE NA KATIBA MPYA

Kama mnavyofahamu, Bunge Maalum la Katiba limeanza vikao vyake Mjini Dodoma tarehe 18 Februari 2014. Wizara iliratibu ushiriki wa Wanadiaspora katika Bunge hilo ili sauti na maoni yao yaweze kujumuishwa katika Katiba Mpya.


Jitihada hizo zimemwezesha mmoja wa Wanadiaspora, Bw. Kadiri Singo kuteuliwan na Mhe. Rais Kikwete, ili kuweza kushiriki kikamilifu. Bw. Singo ameshawasili nchini na kusajiliwa, tayari kushiriki katika Bunge hilo la Katiba Mpya. 


Tunataka Katiba ielekeze kutungwa kwa sheria ya uraia itakayofafanua vigezo na masharti kuhusu haki na wajibu wa Raia wa Tanzania mwenye uraia wa pili; Katiba itamke kuwa raia wa kuzaliwa wa Tanzania hatapoteza uraia wake kwa sababu tu amepata uraia wa nchi nyingine na Katiba ilinde haki ya uraia wa kuzaliwa kwani ni haki ya msingi ambayo haitakiwi kuvuliwa na mamlaka yoyote ile.


FAIDA ZA URAIA WA NCHI MBILI

Tafiti zinaonesha kuwa, Uraia wa Nchi Mbili ni nguzo kuu ya kuandaa mazingira nje ya nchi kuwawezesha raia hao kustawi kielimu, kiafya, kiuchumi, kijamii na kisiasa kama ifuatavyo:

i. Elimu: Elimu ni chimbuko la mafanikio. Uraia wa Nchi mbili utawawezesha kusoma katika shule za Serikali, kulipa ada za chini za raia na kupata ufadhili wa masomo (scholarships).


ii. Ajira: Kupata ajira zenye staha (decent employment). Nchi nyingi hutoa ajira nzuri (au 
katika sekta rasmi) kwa raia pekee hata kama mgeni amesoma na kuwa na sifa sawa au za juu zaidi. Vile vile watanufaika na malipo na huduma zingine uzeeni wakiwa kama raia.

iii. Afya: Afya katika nchi nyingi ni gharama kubwa sana hasa kwa wageni. Kama raia, Watanzania nje ya nchi watanufaika na huduma za afya.


iv. Uchumi: Kama raia, atakuwa na uwezo wa kujishughulisha na masuala ya kiuchumi kwa upana zaidi, kama kupata mitaji mikubwa, kupata mikopo katika taasisi za fedha, kupata zabuni za kibiashara, kumiliki ardhi na mali nyingine ambazo ni kwa raia pakee.

Ushawishi na kuitangaza nchi: Kama raia, Watanzania ughaibuni watakuwa na fursa nzuri na uwezo wa kuisemea Tanzania na kuvutia wawekezaji.


UHAMASISHAJI WA JAMII KUHUSU DIASPORA

Wizaraya Mambo yaNje, kupitia Idara yake ya Diaspora imeanza mchakato wa kuhamasishawa na nchi na kutoa elimu kuhusu masuala ya Diaspora. Hivi sasa, Wizara itaanza kushirikiana na Vyombo vya Habari (radio, televisheni na mitandao ya kijamii) kuongelea umuhimu wa Diaspora katika kukuza uchumi wa Tanzania.

Wizara inasisitiza kuwa taifa lina jukumu la kulinda haki za Watanzania waishio nje kama linavyowajibika kwa raia wanaoishi nchini.

7. MKUTANO KUHUSU KUPINGA BIASHARA HARAMU YA WANYAMAPORI ULIOFANYIKA LONDON, UINGEREZA

Mhe. Rais Jakaya Mrisho Kikwete alihudhuria Mkutano wa Kimataifa wa kuhusu biashara haramu ya wanyamapori. Mkutano huu ulifanyika jijini London, Uingereza kuanzia tarehe 12-13 Februari 2014. Mkutano huu uliandaliwa na serikali ya Uingereza na ulichagizwa na juhudi za Mwanamfalme Charles pamoja na wanae William na Harry katika kushughulikia tatizo hili.


Mkutano uliikutanisha jumuiya ya kimataifa kwa lengo la kujadili na kutafuta mbinu za kumaliza kabisa biashara hii haramu hasa ya pembe za ndovu na faru. Biashara hii imekua sana siku za karibuni hasa kutokana na kuongezeka kwa soko la pembe za ndovu na faru katika nchi za Asia. Uchunguzi wa kimataifa umeonyesha kuwa biashara hii imechukua sura ya kimataifa na kushirikisha magenge ya Kimataifa ya kihalifu kutokana na kuwa na faida kubwa sana. 


Kutokana na kushiriki kwa magenge ya kihalifu ya Kimataifa, biashara hii imehusishwa na kufadhili shughuli za kigaidi, migogoro ya kisiasa na kijamii kwenye baadhi ya maeneo hasa barani Afrika. Mwelekeo huu umeifanya jumuiya ya kimataifa kuanza kuliangalia tatizo la ujangili sio tu kama tatizo la kiuhifadhi (conservation problem) bali pia kama tatizo linalogusa usalama wa Kimataifa (international security).


Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimeathirika sana na biashara hii kutokana na kuwa tembo na faru wengi sana. Ujangili umekuwa ni tatizo sugu kwa nchi yetu tangu enzi za Uhuru mpaka leo. Katika kipindi chote hiki, serikali imeendelea kupambana vikali na majangili kuhakikisha wanyama hawa adhimu wanalindwa na hawapotei katika ardhi yetu. Kwa mfano, baada ya Uhuru Tanzania inakadiriwa ilikuwa na tembo 350,000, kutoka na ujangili uliokithiri katika miaka ya 1980 idadi yao ilishuka na kufikia tembo 55,000 tu mwaka 1987.


Serikali ya wakati huo ikaanzisha operesheni iliyojulikana kama “Operesheni Uhai” ili kupambana na ujangili. Oparesheni hii ilikuwa na mafanikio makubwa na mafanikio haya yalichagizwa pia na marufuku ya biashara ya pembe za ndovu na faru iliyoweka mwaka 1989 na Mkataba wa Kimataifa wa Kuzuia Biashara ya Wanyama walio katika tishio la kupotea(CITES). Kutokana na haya, idadi ya tembo iliongezeka maradufu na kufikia 110,000 mwaka 2009 na ujangili ukawa umedhibitiwa kwa kiwango kikubwa.


Kutokana na kupanuka sana kwa soko la bidhaa hizi hasa kwenye nchi za Asia miaka ya karibuni, wimbi la biashara hii limerudi kwa kasi kubwa sana. Biashara hii imerejea ikiwa na changamoto nyingi sana ikiwemo utumiaji wa mbinu za kisasa kabisa za ujangili. Kama ilivyokuwa huko nyuma kumekuwa na juhudi kubwa sana kwa upande wa serikali kuhakikisha kuwa hali hii, kama ilivyokuwa huko nyuma, inadhibitiwa. Katika juhudi hizo, hivi karibuni Mhe. Rais aliridhia utumiaji wa jeshi letu katika kupambana na kudhibiti biashara hii na hivyo “Oparesheni Tokomeza” ikaanzishwa. 


Kwa bahati mbaya sana kumekuwa na upotoshwaji mkubwa wa juhudi za serikali za kupambana na bishara hii haramu. Baadhi ya magazeti ya Kimataifa yamediriki kuihususha serikali yetu na bishara hii eti kutokana na wao kutokuona uthabiti wa juhudi za serikali kupambana na bishara hii. Tumeenda London kushiriki mkutano huu tukiwa na mambo matatu ya msingi:-


i. Tukiwa miongoni mwa wahifadhi (custodians) wa tunu hii ya wanyama, tumeenda kuungana na jumuiya ya Kimataifa kusaidia kutafuta mbinu za kudhibiti na kumaliza kabisa bishara hii haramu na ambayo inatuathiri sana ukizingatia wanyama hawa nbi kivutio kikubwa cha utalii ambao kwetu moja ya sekta zinazotuingizia fedha nyingi za kigeni.
ii. Kubadilishana mbinu na kuweka kumbukumbu sawa kwa kuelezea juhudi ambazo serikali yetu inazifanya katika kudhibiti biashara hii.

iii. Kuomba usaidizi wa kimataifa pale ambapo juhudi zetu binafsi zinakinzwa na uhaba wa rasilimali, ukosefu wa mbinu za kisasa, ujuzi na uzoefu.

Mkutano ulikuwa na mafanikio sana ambapo Mhe Rais alopata fursa ya kuhutubia. Katika hotuba yake aliungana na viongozi wa kimataifa kupongeza juhudi za serikali ya Uingereza kuitisha mkutano huu muhimu kwenye muda mnuafaka. Katika hotuba yake, pamoja na kuelezea juhudi ambazo serikali yake inazifanya, alisisitiza umuhimu wa kuhakikisha kuwa soko la bidhaa hizi huko katika nchi za Asia linatokomezwa kabisa kama moja ya njia za kuimaliza biashara hii. Pia aliezea juhudi ambazo serikali ya Tanzania imekuwa ikifanya kuhakikisha kuwa tembo na faru waliopo wanalindwa na wanapewa mazingira ya kuzaliana.


Mkutano ulikubaliana pamoja na mambo mengine, kuongeza ushirikiano wa Kimataifa katika kudhibiti bishara hii; kupiga marufuku ya jumla ya bishara hii kimataifa bila kutoa ahueni (moratorium) kama ilivyokuwa inafanyika awali; kuhakikisha kuwa nchi zinapitisha sheria kali dhidi ya ujangili na kuhakikisha kuwa hazina ya meno yaliyohifadhiwa sasa hivi yanakosa thamani (putting stock pile beyond economic use).


8. MAANDALIZI YA MICHEZO YA JUMUIYA YA MADOLA


Michezo ya Jumuiya ya Madola (Commonwealth Games) itafanyika Glasgow, Scotland kuanzia tarehe 23 Julai hadi 3 Agosti 2014.

Miongoni mwa alama kuu za michezo hiyo ni Kifimbo cha Malkia (Commonwealth Queen’s Baton) ambacho hukimbizwa kwa nchi wanachama wa Jumuiya ya Madola kuashiria kuanza kwa michezo hiyo. Kifimbo kicho kilikuja hapa nchini kuaniza tarehe 18 hadi 20 Januari 2014 na kupokelewa na Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Tukiwa na lengo la kuitoa nchi yetu kimasomaso na kufanya vizuri kwenye michezo hiyo, Tuliiomba Serikali ya Uturuki wanamichezo wetu waweke kambi nchini humo kwa ajili ya kufanya maandalizi ya michezo hiyo. Uturuki imekubali ombi hilo. Kwa jitihada hizi za serikali na jitihada za Tanzania Olympic Committee (TOC), pamoja na zile za wanamichezo wenyewe tunategemea wanamichezo wetu watafanya vizuri kwenye mashindano hayo.

Mkwassa kurejea leo na mbinu za kuwadunda Al Ahly

$
0
0


Na Kambi Mbwana, Dar es Salaam
KOCHA msaidizi wa klabu ya Yanga, Charles Boniface Mkwassa, anatarajia kuwasili leo akitokea nchini Misri, akiwa na mipango kabambe ya kuwaangamiza wapinzani wao, timu ya Al Ahly.
Kocha msaidizi wa Yanga, Boniface Mkwassa, pichani.

Mkwassa anarejea Tanzania, akitokea nchini humo kuwasoma Al Ahly, ambayo wataavana nayo Februari 28 mwaka huu katika Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, ukiwa ni mchezo wa kwanza wa mzunguuko wa pili baada ya kuwaondosha Komorozine, ya Comoro kwa bao 12-2.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Msemaji wa Yanga, Baraka Kizuguto, alisema kwamba timu yao ipo vizuri kuelekea kwenye mechi hiyo ya Kimataifa ya Ligi ya Mabingwa Afrika, huku wakikutana na timu ngumu.

Alisema jambo hilo liliwafanya wajipange imara, ikiwapo kumtuma Mkwassa kwenda Misri kufuatilia nyendo za Al Ahly kabla ya kukutana nao uwanjani.

“Mkwassa amepewa jukumu la kuiangamiza Al Ahly ya Misri, katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Afrika, ambapo tunaamini baada ya kurejea kesho (leo), benchi la ufundi litajua wapi kwa kuanzia.

“Tunaomba tuwe na uvumilivu kwakuwa watu wote tuna shauku ya kuona Yanga inasonga mbele katika michuano ya Kimataifa, maana ndio dhamira yetu,” alisema Kizuguto.

Yanga ndio timu pekee ya Tanzania Bara ambayo inaendelea na michuano ya Kimataifa, baada ya kuifungasha virago timu kibonde ya Comoro kwa bao 12-2.



Biashara ya ngono Ziwa Victoria, yadaiwa kuwa wanawake wanalazimishwa penzi ili wapate samani nchini Kenya

$
0
0
Katika ufuo wa bahari ya Ziwa Viktoria kuna biashara inayovuma-dau za uvuvi zilizotengenezwa kwa mbao zimejaa si haba, asubuhi zimejazwa Samaki wa Tilapia.Nyakati za asubuhi na mchana, wavuvi hukusanyika na kupiga foleni kununua Samaki; wengi wao wakiwemo wanawake ambao wanatumainia kupata faida; japo kidogo, katika soko lililo karibu.
Ila, katika sehemu hii ya Kenya, biashara hii haifanywi kwa ubadilishanaji wa pesa kwa Samaki. Malipo ni ubadilishanaji wa ngono kwa Samaki: wanawake wanauza miili yao kwa matumaini kuwa wataeleka nyumbani na Samaki wengi.

Biashara hii inajulikana kama “ubadilishanaji wa ngono kwa samaki” ama, kwa lugha ya kiluo, inajulikana kama “jaboya”. Lucy Odhiambo, 35, anatayarisha ununuzi wake wa mwisho, ambao ataupeleka sokoni; anawapasua samaki na kuwatoa uchafu wa tumboni. Ni mjane, na mama wa watoto tano, anasema kuwa wanawake hapa wanalazimika kufanya wasiyotarajiwa kufanya na jamii.


"Inanilazimu niuuze mwili wangu kwa wavuvi ili nipate samaki kwa sababu sina uwezo wa kujikimu", anaiambia BBC."Kawaida, mimi hulala na wavuvi wawili au watatu kwa juma. Naweza pata magonjwa, ila sina budi kufanya hivyo. Nina watoto ambao nafaa kuwalipia karo. Jaboya ni tendo baya mno. "  

Ugonjwa anaouongelea hapa ni ukimwi ambao umeenea sana katika eneo hili. Ripoti za afya zinadhihirisha kuwa ugonjwa wa Ukinmwi umekithiri katika eneo hili ukiipiku kwa 15% maradufu ile idadi ya wastani ya nchi. Hii inatokana na biashara hii ya “ubadilishanaji wa ngono kwa samaki.Japo polepole, tabia hii inabadilika, huku ikielekea kuisha.
‘Hatutegemei tena wanaume’
Agnes Auma ananipileka ufuoni mwa bahari katika dau analomiliki. Dau hilo linatumiwa na wavuvi ambao amewaajiri kazi, na wanapovua Samaki, yeye ndiye hufanya uuzaji.
Anawalipa wafanyakazi wake na pia gharama za huduma za dau lake, kisha anasalia na hela kadhaa za kujikimu.Mradi unaoendeshwa na shirika la uthamini la eneo hilo linalooitwa Vired unapata msaada kutoka kwa shirika la Marekani la US Peace Corps, na umeweza kuyabadilisha maisha ya wanawake katika eneo hilo.
Tunapiga gumzo wakati dau linazidi kuingia ndani ya ziwa , huku likipita juu ya magugu, na mimea ya baharini, jitihada inayowafanya wavuvi kuloa jasho."Niliona kuwa ningekufa iwapo ningeendelea kuuza mwlili wangu kwa minajili ya kupata samaki-na singeendelea,” Bi. Auma alisema.
“Mradi huu unanisaidia kupata riziki yangu, hivyo basi, si lazima niwategemee wanaume kujikimu. Na, ninapolipia gharama za huduma za dau, nafanya hivyo nafsi yangu ikiwa safi na tulivu.” Tunapofikia sehemu Fulani ndani ya ziwa, wavu unatupwa majini.
Dakika chache baadaye, wavu unatolewa ukiwa umejaa Samaki.Kisha, samaki mkubwa wa kamongo anainuliwa na kutupwa ndani ya dau, huku Bi. Auma akitazama.“Nina furaha kubwa kutokana na jitihada za wavuvi wangu, pia nina furaha kuwa mimi ni mvuvi wa kike ambaye ana bidii na nguvu,” anasema huku akitabasamu.
Leo hii, mradi huu wa Vired, una idadi ya wanawake 19, ila shirika hilo linatumai kuwa idadi hii itaongezeka kadiri muda utakavyoendelea. "Ubadilishanaji wa ngono kwa Samaki ni biashara yenye hatari kwa sababu, kila siku tunagundua kuwa watu wanakufa kutokana na ugonjwa wa Ukimwi,” anasema Dan Abuto wa shirika la Vired.
"Tunahitaji kuwainua wanawake hawa kiuchumi, kinafsi na pia kijinsia ili waweze kupata namna ya kujikimu na kujisimamia. Tuna furaha kuwa mradi huu unavuna matokeo mazuri, na pia wanawake hawa wanadhihirisha bidii na utashi.”
‘Nina aibu’
Ila, hii ni sehemu moja tu ya nchi yangu ambayo “jaboya” ni maarufu. Na hata hapa, kuna wale wavuvi ambao wanafurahia wakilipwa kwa pesa. Lucy Odhiambo: "Nalazimika kulipia samaki kwa kuuza mwili wangu kwa sababu sina namna nyingine ya kujikimu” 
Nakutana na Felix Ochieng, 26, mvuvi ambaye ameoa ila bado anajihusisha na matendo ya ngono nje ya ndoa na wanawake wengine watatu kwa juma, huku akiwapa samaki. Ananiambia kuwa mwanamke atalipia samaki wa shilingi 1000 kwa pesa taslimu ya shilingi 500 ($6; £3.50), huku akitumia mwili wake kujaza akiba ya hiyo shilingi 500 nyingine iliyosalia.
“Niilirithi tabia hii kutoka kwa babangu mwenye alikuwa akifanya vivi hivi," anasema, huku akiapa kuwa anatumia kinga.Namuuliza iwapo ana aibu kutokana na kile anachofanya.
"Ndiyo, nina aibu,” anajibu huku akiangalia upande wa ziwa, “na ni tendo ovu. Ila, kuna matamanio yanayotokana na wanawake." Bado kuna kazi kubwa inayotarajiwa kufanywa ili kuimaliza tabia hii ambayo imekita mizizi katika sehemu kadhaa nchini.
Ila japo kidogo kila siku, idadi ya wanaoshiriki tabia hii inapungua, na wanawake wanaoishi katika maeneo ya ziwa Viktoria wanapata kujua hatari zinazotokana na biashara hii.Kuimaliza biashara hii ya “ubadilishanaji wa ngono kwa samaki” kabisa, tutahitaji kubadilisha fikra na mitazamo yetu, ili kuweza kupata mtazamo mzuri ulio faafu wa jinsia zote.
Na hiyo itakuwa ngumu kufanikisha; kikwazo cha kuweza kufanya biashara ya ubadilishanaji wa samaki kuwezeshwa na pesa pekee.
MAKALA HAYA YAMEANDALIWA NA SHIRIKA LA HABARI UINGEREZA, BBC

Wilaya Kilindi yapania kumaliza migogoro ya wakulima na wafugaji

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, Kilindi

MKUU wa Wilaya Kilindi, Seleman Liwowa, amesema kwamba juhudi za kukomesha migogoro inayoweza kuichafua amani kwenye wilaya hiyo mkoani Tanga, inawekwa kwa kuhakikisha inawaweka sawa wakulima na wafugaji.
Mkuu wa wilaya Kilindi, Selemani Liwowa, pichani.
DC Liwowa aliuambia mtandao huu wa Handeni Kwetu kuwa miongoni mwa migogoro hiyo tishio inasababishwa na wakulima na wafugaji, sanjari na ongezeko la watu wilayani humo na Tanzania kwa ujumla.



Alisema kuwa ofisi yake kwa siku kadhaa sasa imejaribu kukaa na kuliangalia kwa kirefu suala hilo, hivyo anaamini watalipatia ufumbuzi kwa manufaa ya Kilindi na Tanzania kwa ujumla.


“Tumegundua kuwa migogoro hii inasababishwa na wakulima na wafugaji, huku chanzo pia kikiwa ni ongezeko la watu huku ardhi ikiwa haijapimwa.


“Nadhani tumekaa na kuona tupitie upya matumizi ya ardhi kwa upande wa wakulima na wale wafugaji ili kuhakikisha kuwa utulivu unakuwapo wilayani hapa,” alisema.


Kilindi inatokea ubavuni mwa wilaya ya Handeni, mkoani Tanga, ambapo kwa sasa inaongozwa na DC wake Muhingo Rweyemamu, ndani ya Mkoa wa Tanga, ambapo p/ia upo chini ya Chiku Gallawa.

Maandalizi ya uzinduzi wa albamu ya Extra Bongo yakamilika, kesho hapatoshi Dar Live

$
0
0
 Mkurugenzi wa Extra Bongo, Ally Choki akizungumzia uzinduzi wa albamu yao utakaofanyika kesho katika Ukumbi wa Dar Live, Mbagala, jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Ramadhan Masanja, Banza Stone akiafutiwa na Super Nyamwela.
 Wacheza shoo wakicheza katika moja ya maandalizi ya tukio lao la kesho.
 Hapo vipi. Kama kawaida.....
Utawataka vijana wa Extra Bongo, kesho patakuwa hapatoshiiii.

Paulo Makonda apinga kudai nyongeza ya posho katika Bunge la Katiba

$
0
0
Paulo Makonda, pichani.
Mjumbe wa Bunge la Katiba, Paulo Makonda, ametoa ukimya kwa kuelezea kuwa hajatoa tamko lolote linalohusu kudai nyongeza ya posho kama inavyodaiwa na baadhi ya Watanzania juu ya sakata hilo.

Na haya ndio mandishi yake.

Huko nyuma niliwahi kutoa maelezo kuwa kazi tuliyopewa ni ya watanzania na inahitaji muafaka wa kitaifa ili tupate Katiba itakayokidhi mahitaji na matarajio ya watanzania,Katiba bora itakayojali haki na usawa kwa ustawi wa Taifa letu kwa zaidi ya miaka 50 ijayo.
Kuna baadhi ya watu wameanza kujivika uwakala wa kuwa wasemaji wangu, tena kwa nia ya kutaka kuniondoa katika ajenda hii ya msingi kwa maslahi ya watanzania. 


Nimekuwa nikipigiwa simu na kupokea meseji kuhoji juu ya taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao kuwa ninadai ongezeko la POSHO. 


Naomba ieleweke kwamba sijazungumza na chombo chochote cha habari wala kuandika kwenye mitandao ya kijamii kuhusu suala la posho. Taarifa zilizosambazwa kuhusu mimi sio sahihi. Najitambua na natambua wajibu wangu kwa taifa na kwa watanzania wote katika mchakato huu. Natambua hali ya maisha ya watanzania na natambua matarajio yao kwetu, sijateuliwa kuwa mjumbe ili nipate maslahi binafsi ya kiuchumi bali kushiriki katika kuamua mustakabali wa Tanzania tunayotaka kuijenga. 

Hatuwezi kuwa na azma ya kupunguza pengo kati ya walionacho na wasionacho, huku tukiendelea kudai maslahi makubwa zaidi kwa WABUNGE na wawakilishi na kusahau maslahi ya wanyonge walio wengi.
Nawaomba vijana wenzangu na wale wote wanaosambaza taarifa hizo, badala ya kutumia muda mwingi kuandaa majungu na fitina, tumieni muda vizuri kutushauri mambo ambayo sote kwa pamoja tunadhani yatasaidia kuliendeleza Taifa letu kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Salamu za TAWODE katika mafunzo ya Utawala bora jijini Tanga

$
0
0
Mheshimiwa Mgeni Rasmi, Naibu Waziri , Ofisi ya Makamu wa Raisi, Mazingira,  Ummy Ally Mwalimu, Wakuu wa Wilaya, Waheshimiwa Madiwani wanawake  kutoka Halmashauri Mbalimbali, Watendaji wa serikali, Ndugu wawezeshaji, Waandishi wa Habari na Ndugu washiriki,  namshukuru mungu kwa kutuamsha na kukutana pamoja siku ya leo.

Habari za asubuhi na karibuni sana katika Mafunzo ya Uongozi na Utawala Bora (kwa ajili ya Maendeleo ya Wanawake na watoto) kwa waheshimiwa madiwani wanawake kutoka Wilaya nane za Mkoa wa Tanga ambazo ni Mkinga, Muheza, Korogwe,  Lushoto, Handeni, Kilindi, Pangani na Tanga.

Tunawashukuru sana kwa kuitika wito wetu na kuja  kushiriki katika mafunzo haya. Pia tunawashukuru watendaji wa Halmashauri waliofanikisha upatikanaji wa washiriki wetu kwa kutambua umuhimu wa mafunzo haya kwa maendeleo ya Wanawake na Taifa letu la Tanzania. Ni jambo jema kushirikiana pale kunapokua na jambo la kimaendeleo ambalo linahitaji ushiriki wa taaluma, uzoefu na mitizamo mbalimbali. Asanteni sana.  

Kwa namna ya pekee niwashukuru Viongozi wa Serikali na Madiwani  ambao wametoka Wilaya mbalimbali kuja kuhudhuria warsha  huu. Poleni kwa safari na niwatakie safari njema mtakapokua mnarudi.


Kama tunavyojua TAWODE  ni Taasisi isiyo ya kiserikali iliyoanzishwa na kikundi cha wanawake wa Mkoa wa Tanga ikiwa lengo ni kuchochea Hamasa ya maendeleo kwa wanawake wa Mkoa wa Tanga mwaka 2011. Na leo tunafurahi kuendelea na  utekelezaji wa shughuli za  Taasisi . 

 Lengo likiwa ni Kuboresha hali za  Kiuchumi na Kijamii za Wanawake na Watoto katika Mkoa wa Tanga na Kuchochea hamasa ya Masuala ya Usawa wa Jinsia, Haki za Watoto na Maendeleo ya Jamii ndani na nje ya Mkoa wa Tanga. Mafunzo haya yanajumuisha Washiriki 93 kutoka Wilaya za Mkinga, Pangani, Korogwe, Muheza, Lushoto,Handeni, Kilindi na Tanga. 

 Madhumuni ya mafunzo haya ya siku tatu ni Kuchochea ongezeko la mchango na ushiriki wa waheshimiwa Madiwani Wanawake katika kusimamia na kutetea maamuzi na Utekelezaji wa Mipango ya Maendeleo katika Serikali za Mitaa hasa ihusuyo afya ya uzazi, Maji, Utawala Bora, Elimu kwa watoto wa Kike na Upatikanaji wa Mitaji kwa ajili ya shughuli za kuwaongezea wanawake kipato.  Mafunzo mtakayoanza leo ni muendelezo wa kazi zenu za utendaji wa kila siku. 

 Aidha napenda kusema kwamba Mafunzo mtakayopata katika semina hii yataenda sambamba na jitihada za Serikali katika kumwezesha kila mshiriki, sio tu katika maamuzi kwenye ngazi ya familia, bali hata katika ngazi mbalimbali katika jamii na taifa kwa ujumla, katika nyanja mbalimbali za maendeleo kama vile kuanzisha vikundi mbalimbali vya wasichana vya ujasirimali na vya kujadili masuala mbalimbali yanayogusa maendeleo yao ikiwemo kukataa maambuzi ya VVU/UKIMWI, kukataa mimba za mapema, ndoa za mapema na pia kuhimiza kujituma kufanya kazi, kuwahimiza kujitahidi katika masuala ya elimu.  

Hivyo basi tunawaomba washiriki wetu muwe huru  kutoa ushirikiano katika mafunzo haya. Tunaamini mafunzo haya yatawasaidia na kuwaongezea  nguvu ya kuleta mabadiliko katika jamii zetu. Tunatarajia mafunzo haya yatasaidia kuwapa moyo wanawake wengine kushiriki katika nafasi mbalimbali za uongozi na kuleta mabadiliko katika jamii na Taifa kwa ujumla.
Nawashukuru sana Viongozi na waheshimiwa  Madiwani wanawake kutoka Halmashauri mbalimbali za Mkoa wa Tanga. Mhe Mgeni Rasmi, Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Raisi, Mazingira Ummy Mwalimu sasa nikuombe rasmi uje utufungulie mafunzo yetu.

Ligi ya Tanzania Bara kuendelea tena kesho

$
0
0
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
LIGI Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara inaingia raundi ya 19 kesho (Februari 22 mwaka huu) kwa mechi tano zitakazochezwa katika miji ya Dar es Salaam, Bukoba, Morogoro, Tanga na Arusha.


Yanga itakuwa mgeni wa Ruvu Shooting ya mkoani Pwani katika mechi itakayofanyika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Nayo Kagera Sugar inaikaribisha Rhino Rangers ya Tabora katika mchezo utakaofanyika Uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.


Uwanja wa Manungu uliopo Turiani mkoani Morogoro ndiyo utakaotumika kwa mechi kati ya Mtibwa Sugar na Ashanti United, wakati Coastal Union itaumana na Mbeya City katika mechi itakayooneshwa moja kwa moja na Azam Tv kutoka Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga.


Maafande wa Oljoro JKT watakuwa nyumbani kupambana na Mgambo Shooting katika mchezo utakaofanyika kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid jijini Arusha.


Jumapili (Februari 23 mwaka huu) katika Uwanja wa Taifa ni Simba dhidi ya JKT Ruvu, mechi ambayo pia itaoneshwa moja kwa moja na Azam Tv. Mechi kati ya Azam na Tanzania Prisons iliyokuwa ichezwe kesho (Februari 22 mwaka huu) Uwanja wa Chamazi sasa itachezwa Jumapili (Februari 23 mwaka huu) ambapo na itakuwa ‘live’.


Ligi hiyo itaendelea Jumatano (Februari 26 mwaka huu) kwa mechi moja kati ya Ashanti United na Azam itakayochezwa kwenye Uwanja wa Azam Complex (Chamazi).

Uchaguzi wa Kamati ya Utendaji ya TASWA kufanyika Machi 2 mwaka huu

$
0
0

Uchaguzi wa Kamati ya Utendaji ya Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA) utafanyika Machi 2, 2014 jijini Dar es Salaam. 


Kwa mujibu wa taarifa zilizoifikia Tanga Raha blog kupitia Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi huo,Boniface Wambura zimeelewa kuwa fomu kwa ajili ya waombaji uongozi zinaanza kutolewa Jumatatu (Februari 24 mwaka huu) kwenye ofisi za Idara ya Habari. 

Mwisho wa kuchukua na kurudisha fomu ni Alhamisi (Februari 27 mwaka huu) saa 9 alasiri.


Ada kwa wagombea wa nafasi za Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mhazini na Mhazini Msaidizi ni sh. 50,000 kwa fomu. Nafasi za wajumbe wa Kamati ya Utendaji fomu zinapatikana kwa sh. 20,000.

Kamati ya Uchaguzi inawahimiza wanachama wa TASWA kujitokeza kwa wingi kugombea, lakini vilevile waisome vizuri Katiba ya chama chao.

Matokeo kidato cha nne yatangazwa, angalia majina ya shule zilizofaulisha vizuri

$
0
0
Matokeo ya kidato cha nne mwaka 2013 yametangazwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi leo jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa Wizara hiyo, shule 10 bora zilizopata matokeo mazuri ni pamoja na 1. St.Francis Girls (Mbeya), 2. Marian Boys (Pwani), 3. Feza Girls (Dar-es-salaam), 4. Precious Blood (Arusha), 5. Canossa (Dar-es-salaam), 6. Marian Girls (Pwani), 7. Anwarite Girls (Kilimanjaro), 8. Abbey (Mtwara), 9. Rosmini (Tanga) na 10. DonBosco Seminary (Iringa).

MATOKEO YA KIDATO CHA NNE MAPYA HAYA HAPA 2013

NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA

ACSEE 2013 EXAMINATION RESULTS ENQUIRIES




































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































Viewing all 1305 articles
Browse latest View live